» »Unlabelled » Aliyetobolewa macho Buguruni Sheli apelekwa Muhimbili

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda Jumapili hii aliahidi kumkutanisha Said Ally aliyepoteza uwezo wake wa kuona Buguruni Sheli jijini Dar es salaam, na leo hii amemkutanisha na madaktari wa Muhimbili.

Said Ally amechukuliwa Jumatano hii nyumbani kwake na gari ya mkuu wa mkoa na kupelekwa moja kwa moja katika hospitali hiyo.

Makonda ameandika kwenye Instagram, “Nawashukuru madaktari bingwa kutoka hospitali ya Muhimbili, kwa kazi kubwa wanayoifanya kumsaidia ndugu yangu Said Ally Mrisho apate kuona tena, nawaomba tuendelee kumuombea”, aliandika Makonda.

Mkuu huyo wa mkoa, amejitolea kumsaidia kijana huyo.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post