Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Yusuf Masaun leo amefanya ziara ya ghafla katika kituo kikuu cha mabasi Ubungo na kufanya ukaguzi wa mabasi pamoja na kituo kidogo cha Maili Moja na kulazimika kusitisha safari za mabasi mawili kutokana
Baada ya kufika katika kituo cha Ubungo Mh. Masauni aliamuru basi la Shambalai linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Lushoto lenye namba za usajili T419 BUF, pamoja na basi la kampuni ya Karachani lenye namba za usajili T253 CLZ na kutaka yasitishe safari baada ya kutokidhi vigezo vya kusafirisha abiria.
Aidha Masauni ametoa wiki moja kwa maofisa wa usalama barabarani Mkoani Pwani kuhakikisha wanafanya mabadiliko ya ukaguzi wa mabasi katika kituo cha mabasi cha maili moja mkoani humo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha kutetea abiria (CHAKUA) Bw. Hassan Mchanjama ameomba kuboreshwa kwa huduma katika kituo cha Ubungo ili kuendana na hadhi yake.
Katika ziara hiyo, Masauni aliongoza na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Naibu Kamishna wa Polisi Mohamed Mpinga .
Baada ya kufika katika kituo cha Ubungo Mh. Masauni aliamuru basi la Shambalai linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Lushoto lenye namba za usajili T419 BUF, pamoja na basi la kampuni ya Karachani lenye namba za usajili T253 CLZ na kutaka yasitishe safari baada ya kutokidhi vigezo vya kusafirisha abiria.
Aidha Masauni ametoa wiki moja kwa maofisa wa usalama barabarani Mkoani Pwani kuhakikisha wanafanya mabadiliko ya ukaguzi wa mabasi katika kituo cha mabasi cha maili moja mkoani humo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha kutetea abiria (CHAKUA) Bw. Hassan Mchanjama ameomba kuboreshwa kwa huduma katika kituo cha Ubungo ili kuendana na hadhi yake.
Katika ziara hiyo, Masauni aliongoza na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Naibu Kamishna wa Polisi Mohamed Mpinga .
