» »Unlabelled » Wanaswa na meno ya tembo wakitafuta soko, Njombe

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Kamanda wa Polisi mkoani Njombe Pudensiana Protas

Jeshi la polisi mkoani Njombe linawashikilia vijana wawili wakazi wa mkoa jirani wa Iringa wakiwa na meno sita ya Tembo yenye uzito wa kilo 13.6 ambayo walikuwa katika harakati za kutafuta wateja.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Njombe Kamanda wa Polisi mkoani humo Pudensiana Protas amesema kuwa vijana hao wawili walikuwa na pikipiki ambapo polisi wakiwa doria katika kijiji cha Kitandililo wilaya ya kipolisi Makambako waliwakamata vijana hao baada ya kuwatilia shaka.

Kamanda Protas amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Emanuel Lyabonga na Thomas Mhomba wakazi wa Iringa na kwamba wamekamatwa na jeshi hilo wakiwa na pikipiki yenye namba za usajili MC 916 AWN.

Kuhusu thamani ya meno hayo Protas amesema kuwa wanasubiri wataalamu kutoka Idara ya maliasili ili kutambua thamani yake huku akitoa wito.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post