» » Wasafiri 300 wakwama Ubungo

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Dar es Salaam. Zaidi ya wasafiri 300 leo  wamekwama kusafiri katika kituo cha mabasi ya mikoani Ubungo baada ya kujitokeza hitilafu katika mabasi matano.

Katibu wa Idara ya Barabara kutoka Chama cha Kutetea Abiria(Chakua), Godwin Ntongeji alisema mabasi yalitakiwa kuanza safari zake saa 12:00 asubuhi kwa mujibu wa ratiba za Mamlaka ya Usafiri wa Nchi kavu na Majini (Sumatra).

 “Tangu saa 12 asubuhi abiria wamekwama kuondoka , yapo ambayo yanaendelea kufanyiwa matengenezo ili yaondoka, ukaguzi umeongezeka kwa sasa lakini abiria wanaumizwa sana kwani haiwezekani wakala wa basi akatishe tiketi kumbe basi bovu,”alisema huku akiwa amezungukwa na abiria wanaohitaji msaada kutoka ofisi yake.

Gazeti hili limeshuhusia baadhi ya mabasi hayo yakiwa yanafanyiwa matengenezo huku abiria wakilanda landa na wengine wakihitaji msaada wa mamlaka husika.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post