» » Mwili wa dereva wa mbio za magari aliyefariki akikwea mlima Kilimanjaro wawasili SA

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

 Mwili wa dereva wa mbio za magari wa Afrika Kusini aliyefariki wakati akikwea mlima Kilimanjaro, Gugu Zulu umewasili jijini Johannesburg kwaajili ya mazishi.

Zulu alifariki wiki hii akipanda mlima huo akiwa pamoja na mke wake na raia wengine wa Afrika Kusini.

Alikuwa sehemu ya timu ya Trek4Mandela iliyoshiriki zoezi hilo kuchangisha fedha kusaidia wasichana maskini. Timu hiyo ilirejea Afrika Kusini usiku wa Jumatano hii.

Mwili wake uliwasili jana usiku na taratibu za kutoa heshima ya mwisho na mazishi zinafanywa.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post