Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dk Juliana Pallangyo.
Akifungua Kongamano la Tatu la Wadau Gesi ya Kupikia (LPG) barani Afrika, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dk Juliana Pallangyo amesema mpango huo utaanza kutekelezwa Septemba.
“Changamoto iliyopo ni gharama kubwa. Uagizaji wa pamoja utashusha bei na kila Mtanzania atamudu. Hii itasaidia kuokoa misitu kwa kupunguza matumizi ya kuni na mkaa,” amesema.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Ununuzi wa Pamoja Mafuta na Bidhaa zake (PBPA), Michael Mjinja amesema jukumu lililo mbele yake ni kuisimamia sekta hiyo ili iwe na manufaa kwa kila mwananchi.
