» » Waziri: Ugatuzi wa madaraka tatizo bungeni

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO




Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene
Dodoma. Wabunge wengi wanajadili hoja nje ya muktadha kwani wengi hawafahamu sawasawa namna ambavyo dhana ya ugatuzi wa madaraka (DBD) inavyofanya kazi, Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene amesema.
Simbachawene amesema hayo leo asubuhi wakati wa kipindi cha maswali na majibu bungeni baada ya kubaini namna ambavyo wabunge wanavyojichanganya katika suala hilo.
“Wengi wanataka Serikali irudi kwenye mfumo wa Serikali Kuu kufanya kila kitu…hii ina maana wengi hawaelewi maana ya DBD (ugatuzi wa madaraka),” Simbachawene amesema kuna umuhimu ya wabunge hao kuandaliwa semina juu ya suala hilo.
Amesema Taasisi ya Uongozi itashirikishwa katika mafunzo hayo, jambo ambalo limeungwa mkono na Naibu Spika Tulia Ackson aliyeitaka Serikali kulitaarifu Bunge mara maandalizi yatakapokamilika.
Alipoulizwa iwapo mafunzo hayo yataleta tija katika dhana nzima ya ugatuzi wa madaraka, mtafiti kutoka Twaweza, Richard Lucas amesema mafunzo siyo tatizo pekee bali Serikali inapaswa kuhakikisha ugatuzi unatendekea katika Serikali za mitaa.
Akitolea mfano namna bajeti zinavyotengenezwa kuanzia ngazi ya vijiji na fedha zinazotengwa kwa ajili ya utekelezaji na uchangishaji wa madawati nchi nzima, ofisa huyo amesema ni miongoni mwa masuala yanayodhihirisha Serikali kuhodhi baadhi ya mambo ambayo ni kikwazo kwa utekelezaji wa DBD.
“Kuna hili suala la uchagiaji wa madawati nchi nzima, mimi nimetembea katika shule kadhaa Kilimanjaro, suala hilo siyo tabu kwa shule nyingi, lakini dhana ya DBD ingekuwa inatekelezwa hakika wengi wa wakazi wa mkoa huo, kipaumbele kingekuwa siyo madawati, huenda kuna jambo tofauti wanalohitaji tofauti na madawati,” ameeleza Lucas.
Mtafiti huyo ameongeza kuwa iwapo wananchi wataibua miradi wanayoihitaji kupitia dhana nzima ya ugatuzi wa madaraka, ni dhahiri itakuwa endelevu kuliko ile inayotoka moja kwa moja Serikali Kuu.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post