» » Watatu wadakwa wakiwa dawa za kulevya, gongo

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Mwanza. Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu watatu wakazi wa maeneo ya Kabangaja–Mnarani, Kata ya Bugongwa wilayani Ilemela wakijihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya na pombe aina ya gongo.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ahmed Msangi amesema watu hao walikamatwa Juni mosi saa 12 jioni wakiwa na kilo mbili, misokoto 12 ya bangi na lita 10 za pombe aina ya gongo, kitendo ambacho ni uvunjwaji wa sheria na taratibu za nchi.

Msangi aliwataja waliokamatwa kuwa ni Leticia Elias (52) mkazi wa Igombe, Thomas Lipovitia (49) mkazi wa Kibagaja na Majani Manyego (38) ambaye alikutwa akiuza gongo.

“Watuhumiwa wote wako chini ya ulinzi kwa mahojiano na uchunguzi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka,” alisema.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post