» » Wastara Aamua Kuachana na Uigizaji

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Dar es Salaam: Staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma amejipanga kuachana na uigizaji na kufanya ishu nyingine ikiwa ni pamoja na biashara ambazo ameanza kuzifanya.

Akizoza na Wikienda, Wastara alisema kuwa anamalizia kazi ya uigizaji mwaka huu na mwaka unaokuja atakuwa mwingine kabisa kwani baada ya kufika nchini Msumbiji (aliko kwa sasa) amepata dili lingine zuri ambalo ataliweka wazi baada ya mipango yake  kukamilika.

“Kinacho niachisha uigizaji si biashara tu bali ni pamoja na dili nililolipata huku Msumbiji, kama litakwenda nilivyopanga, nitaliweka wazi inshallah,” alisema Wastara.

Hivi karibuni, Wastara aliripotiwa kuwa na ujauzito ambapo alikimbilia nchini Msumbiji.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post