» » » Wales 3-0 Urusi

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


 Aaron Ramsey

Wales ilijifurukuta na kuilaza Urusi mabao matatu kwa nunge katika mechi ya mwisho na muhimu ya makundi jana usiku.

Aaron Ramsey na Neil Taylor na Gareth Bale walifunga mabao hayo muhimu na kuisaidia timu hiyo ya kocha Chris Coleman ikiwa imejihakikishia nafasi katika mkumbo wa pili kwa mara ya pili katika historia yake.

 Wales 3-0 Urusi

Wapinzani wao wa jadi England walimudu sare tasa dhidi ya Slovakia mjini Saint-Etienne na kuhakikisha kuwa Wales wanafuzu kwa raundi ya pili ya mashindano hayo kama vinara wa kundi B.

Matokeo hayo yanamaanisha kuwa Wales sasa watachuana na mshindi wa tatu katika kundi C A ama D.

Aaron Ramsey na Gareth Bale

Wales na England zimefanikiwa kusonga mbele katika michuano ya Euro baada ya mechi zake za kundi B kukamilika.

Vijana wa Chris Coleman wamewabamiza Russia mabao 3 kwa 0 na huku England ikija ya pili kwenye kundi baada ya kubanwa mbavu na Slovakia.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post