» » Wakulima wa miwa Kilosa waomba suluhu

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


 

Kilosa.Chama cha Wakulima wa Miwa Bonde la Ruhende (RCGA), wilayani Kilosa wameziomba mamlaka husika kutatua mgogoro wa muda mrefu wa chama hicho ambao umesababisha viongozi waliokuwapo madarakani kuondolewa kwa tuhuma za ubadhirifu.
Mwenyekiti wa muda wa chama hicho Christopher Hembu amesema viongozi wa awali waliondolewa katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Tundu, wilayani humo Machi 3 uliohudhuriwa na Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba.
Katika mkutano huo wajumbe waliwatuhumu viongozi waliokuwamo madarakani kwa ubadhirifu wa mali za chama na kusababisha migogoro ya wakulima na kiwanda cha sukari kilombero hali inayozorotesha maendeleo ya chama.
Hembu amesema katika mkutano huo waziri Nchemba aliwaagiza kupitia na kurekebisha katiba ya chama kwani ilionekana ina upungufu baada ya nafasi za uongozi kuondolewa ukomo hali ambayo pia inasababisha mgogoro.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post