» » Wafa kwa kula chakula chenye sumu

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


 


Simanjiro.Watoto wawili wa familia moja kwenye kitongoji cha Nadosoito wilayani hapa wamefariki dunia na wengine wawili kunusurika baada ya kula maandazi yanayosadikiwa kuwa na sumu.
Baada ya kula maandazi na kusikia maumivu ya tumbo, walipewa dawa za kienyeji za jamii ya wafugaji wa kimasai badala ya kupelekwa hospitalini.
Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Mahmoud Kambona amesema watoto hao walifariki Juni 14 saa 10:00 jioni na kuwataja waliofariki dunia kuwa ni Jonas Zebedayo (17) na John Zebedayo (14), huku Elizabeth Zebedayo (12) na Joshua Zebedayo (11) waliosurika wakiwa wamelazwa Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru wakitibiwa.
Amesema chanzo cha vifo vivyo ni chakula chenye sumu walichokula wakati wazazi wao hawapo nyumbani, lakini akasema wamechukua mabaki hayo na kupeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili uchunguzi ufanyike kubaini chanzo.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post