» » Upinzani: Hatubadili msimamo kwa Dk Tulia

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO



Dodoma. Msemaji wa Kambi ya Upinzani, David Silinde amesema uamuzi wa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuwa wabunge wanaomsusia wasilipwe posho kwa sababu wamekuwa wakisaini na kutoka nje, hauwatishi na wataendelea kufanya hivyo.

“Mbunge akisaini analipwa posho hiyo iko kwa mujibu wa kanuni, sasa yeye Dk Tulia juzi alipotoa mwongozo alianza na kanuni lakini baadaye akaingia kwenye taratibu tofauti, kwamba mbunge akisaini na kutoka hatalipwa, hapo amechemsha,” alisema Silinde.

Alisisitiza kuwa hatua hiyo ni kinyume na utaratibu, kwani kiongozi huyo wa Bunge alitoa hukumu ya kesi inayomhusu yeye mwenyewe.

 “Malipo yawe kwa mtu anayechangia kwa kuwa kuna wabunge wanaingia na kusaini, lakini hawasemi chochote bungeni, kazi yao ni kupiga makofi tu na hawachangii,” alisema.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post