» » Uganda kuwaondoa wanajeshi wake Somalia

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Uganda imeamua kuwaondoa wanajeshi wake kutoka nchini Somalia ifikapo mwezi Disemba mwaka 2017.

Uganda inachangia wanajeshi wengi zaidi kwa kikosi cha muungano wa afrika kinachopigana na wanamgambo wa Al-Shabab.

Mkuu wa jeshi nchini Uganda Jenerali Katumba Wamala, aliiambia BBC kuwa hatua hiyo ilichukuliwa kutokana na hujuma kutoka kwa jeshi la Somalia na washirika wa kimataifa.

Marekani, Uingereza na Uturuki ni kati ya nchi ambazo hutoa mafunzo kwa jeshi la polisi wa Somalia.
Lakini serikali ya Uganda inasema kuwa nchi hizo hazitoi ushirikiano.

Jenerali Wamala anasema kwa Uganda itaondoa jeshi lake kabla ya Disemba mwaka 2017 ikiwa nchi nyinge itapatikana kuchukua mahala pake.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post