Dar es Salaam. Hatimaye Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesalimu
amri kwa kukubalia uchaguzi wa klabu hiyo ufanyike Juni 11 badala ya
25.
Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas alisema jana kuwa uamuzi huo umetokana na kikao kilichokutanisha pande hizo mbili na kufikia mwafaka.
TFF iliwakilishwa na Rais, Jamal Malinzi, Katibu Mkuu, Celestine Mwesigwa na Kaimu Mkurugenzi wa Masuala ya Wanachama na Sheria, Eliud Mvela huku Yanga ikiwakilishwa na Katibu Mkuu, Baraka Deusdedit na Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga.
Lucas alisema kikao hicho kiliridhia mchakato huo wa uchaguzi uendelee huku Malinzi akiagiza kamati ya uchaguzi ya Yanga iwe msimamizi wa uchaguzi huo, huku kamati ya uchaguzi ya TFF ikiwa mwangalizi.
Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas alisema jana kuwa uamuzi huo umetokana na kikao kilichokutanisha pande hizo mbili na kufikia mwafaka.
TFF iliwakilishwa na Rais, Jamal Malinzi, Katibu Mkuu, Celestine Mwesigwa na Kaimu Mkurugenzi wa Masuala ya Wanachama na Sheria, Eliud Mvela huku Yanga ikiwakilishwa na Katibu Mkuu, Baraka Deusdedit na Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga.
Lucas alisema kikao hicho kiliridhia mchakato huo wa uchaguzi uendelee huku Malinzi akiagiza kamati ya uchaguzi ya Yanga iwe msimamizi wa uchaguzi huo, huku kamati ya uchaguzi ya TFF ikiwa mwangalizi.
