» » Polisi Mwanza waua jambazi mmoja, askari ajeruhiwa

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO



Mwanza. Polisi mkoani Mwanza wamemuua jambazi mmoja baada ya kujibizana kwa risasi muda huu.
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ahmed Msangi ambaye yuko kwenye eneo la tukio, amesema katika tukio hilo, askari mmoja amejeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni na jambazi huyo aliyeuawa ambaye alikuwa na mwenzake anayedaiwa kukimbilia kwenye majabali ya mawe.
Amesema majibizano hayo yalianza saa 6.20 katika Mtaa wa Utemini, baada ya polisi waliokuwa doria kufuatilia nyendo za watu hao.
“Tulipokea taarifa kutoka kwa rai wema kuwa katika eneo hilo kuna watu wanaowatilia shaka, ndipo askari wakaamua kuwafuatilia.
Hata hivyo, amesema wamefanikiwa kukamata bastola moja iliyokuwa ikitumiwa na jambazi huyo.
“Unasikia milio hiyo ya risasi, askari wanaendelea kumsaka huyo mmoja aliyejificha kwenye mawe, naimani tutampata tu na hatuondoki hapa mpaka tumtie mikononi,” alisema Msangi na kuongeza:
“Hawa ni majambazi sugu ambao walikuwa wakituhumiwa kufanya matukio uporaji na mauaji jijini hapa, tulikuwa tukiwasaka kwa muda mrefu.”
Kwa taarifa zaidi nunua gazeti lako la Mwananchi au soma mtandaoni kupitia
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post