» » » Koeman sasa ni wazi wa Everton amwaga wino rasmi

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Kocha mpya wa Everton Ronald Koeman
Katika kuhakikisha inafanya vema katika michuano ya msimu ujao timu ya Everton imefanikiwa kuimarisha benchi lake la ufundi mara baada ya kuingia mkataba rasmi na aliyekuwa kocha wa Southampton Ronald Koeman.
Kocha huyo aliyekuwa na mafanikio akiwa na kikosi cha Southampton, sasa ni rasmi ametua kuchukua ujira wa kuinoa Everton msimu ujao utakaoanza mwezi Agosti mwaka huu.

Kocha huyo raia wa Uholanzi anachukua nafasi iliyoachwa na kocha Roberto Martinez ambaye alionyeshwa mlango wa kutokea baada ya kuwa na msimu unaosuasua na vijana hao wanaotumia dimba la Goodson Park.

Taarifa zinaweka wazi kuwa kocha Koeman amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kukinoa kikosi cha timu hiyo na anataraji kuingiza kitita cha paundi million 6, akilipwa kiasi cha paundi million 2 kila msimu kwa mujibu wa mkataba wake huo.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post