» » Kesi ya Chadema dhidi ya polisi yaanza

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO




Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
Mwanza.  Shauri la kupinga amri ya polisi ya kupiga marufuku maandamano na mikutano ya kisiasa iliyofunguliwa na Chadema katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza inaanza kusikilizwa mchana huu baada ya kupangiwa jaji.
Msajili wa wilaya wa mahakama hiyo, Francis Kabwe amesema shauri hilo linasikilizwa na Jaji Mohamed Ngwae.
Katika madai yake ya msingi, Chadema kupitia kwa Mwenyekiti wa wa chama hicho, Freeman Mbowe inaiomba mahakama kutangaza kuwa amri ya polisi ni batili na utekelezaji wake pia ni batili kwa sababu inakiuka katiba na sheria ya vyama vya siasa inayoruhusu uhuru wa mawazo, kukusanyika, kutoa maoni na demokrasia.
Chadema pia inaiomba mahakama kutoa katazo la kimahakama kwa polisi dhidi ya amri kama hizo na pia iviruhusu vyama vya siasa kuendelea na shughuli za kisiasa, ikiwamo maandamano na mikutano ya hadhara huku polisi wakiamriwa kutoa ulinzi kama sheria inavyoelekeza.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post