» » Chadema kuichongea Serikali kwa wananchi

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


 

Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza kuanza ziara nchi nzima ya kuwaelimisha wananchi juu ya ubakwaji wa demokrasia wanakodai kufanywa na Serikali.
Pia, katika ziara hiyo, viongozi wa chama hicho watazungumzia utumbuaji majipu wanaodai kuwa haufuati maadili ya kazi pamoja na kutoonyeshwa kwa matangazo ya moja kwa moja ya televisheni ya vikao vya Bunge vinavyoendelea Dodoma.
Mratibu wa ziara hiyo, Singo Benson alisema ziara itaanza Juni 7 katika Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga na kuendelea mikoa mingine.
“Wananchi wananyimwa haki ya msingi ya kutoona matangazo ya Bunge moja kwa moja na hakuna sababu ya msingi iliyotolewa, hivyo lazima tuwaelimishe na tutetee haki ya wananchi,” alisema Benson.
Aliongeza kuwa katika utumbuaji majipu unaofanyika, umekuwa kwa asilimia kubwa ukilenga majipu madogo (viongozi wa chini) na kuacha viongozi wakubwa mafisadi bila kuchukuliwa hatua yoyote.
Benson alitoa mfano wa ubakwaji wa demokrasia akisema ni kitendo cha Serikali kuingilia mihimili mingine, Bunge na Mahakama, ambapo kwa Bunge Serikali inadaiwa kuingilia uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ambaye anatakiwa kutoka kambi ya upinzani.
Alisema ziara hiyo itamjumuisha Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wake, Dk Vincent Mashinji, itakuwa na awamu nne huku wabunge wote na wajumbe wakuu wa chama watashiriki, akiwamo aliyekuwa mgombea urais 2015, Edward Lowassa.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post