» » Baraza la Famasia lakamata dawa za Sh337 milioni

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Dar es Salaam. Baraza la Famasia Tanzania wamekamatwa dawa zenye thamani ya Sh337 milioni baada ya kufanya operesheni ‘Safisha’ katika maduka ya mikoa tisa nchini ambayo  yalifunguliwa bila kufuata utaratibu.

Msajili wa baraza hilo, Elizabeth Shikalage amesema wanaofanya biashara ya dawa bila kufuata utaratibu wanavunja Sheria ya Famasia, Sura 311 pamoja na Sheria za nchi katika uendeshaji wa utoaji wa huduma za dawa.

Amesema walikagua maduka ya dawa 685, kati ya hayo, 432 yalifungiwa kutokana na ukiukwaji wa sheria ya uanzishaji na uendeshaji.

Amesema dawa zinazofaa kwa matumizi ya binadamu zina thamani ya Sh325 milioni na zisizofaa   Sh11.2 milioni. 
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post