» » Baada ya kuoa mwanamke mwingine, Isabella adai ni yeye ndiye alimpiga chini Kalama, adai ni mwanaume asiye na future

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Baada ya rapper wa kundi la Gangwe Mobb, Luteni Kalama kuoa mwanamke mwingine na kumwacha mchumba wake aliyemvisha pete, Isabella ameibuka na kudai kuwa ni yeye ndiye aliyemwacha baada ya kumuona ni mwanaume asiye na future.

“Mimi na Kalama tulikuwa tumeshaachana muda mrefu kwasababu nimeona ni mwanaume ambaye hana future hawazi chochote, kwahiyo nikaona kwanini nijipotezee muda. Mwanaume anaamka saa saba, kwahiyo nikaona niachane naye,” Isabela alimuambia mtangazaji wa Jembe FM, Natty E.

“Lakini watu wameona ilivyotokea gazeti wanahisi labda Kalama aliniacha mimi kitu ambacho sio kweli, hana uwezo wa kuniacha, mimi ndio nilimuacha. Na nafikiri stress zake ndio zimemfanya aende akamuoe rafiki yangu sasa si ni uchizi. Halafu mwanamke unaoa unaenda kukaa kwa mwanamke tena, yeye si ndio anakuwa ameolewa, kwahiyo yeye ni mwanaume ambaye ni kilaza,” aliongeza Isabela.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post