» » Aliyewaua wanawake 10 kunyongwa

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Lonnie David Franklin Junior alipatikana na hatia mwezi uliopita

Jopo la waamuzi mjini Los Angeles, limeamua kuwa mshukiwa mmoja ambaye alipatikana na hatia ya mauaji, anayefahamika kama 'Grim Sleeper', anapaswa kuhukumiwa kifo.

Lonnie David Franklin Junior alipatikana na hatia mwezi uliopita, ya kuwaua wanawake tisa na msichana mmoja mwenye umri wa miaka kumi na mitano katika kipindi cha miaka ishirini iliyopita.

Franklin junior alifahamika kama Grim Sleeper kwa sababu alitekeleza mauaji mengine baada ya miaka kumi na mitatu.

Aliwalenga wanawake masikini na wasichana wachanga ambao aliwaua na kutupa miili yao kwenye pipa za taka na mitaro ya kupitishia maji machafu.

Mshukiwa huyo sasa atakabithiwa hukumu yake agosti mwaka huu.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post