Kwa sasa Mayunga anafanya vizuri na wimbo wake wa ‘Please Don’t Go Away’ aliomshirikisha msanii kutoka Marekani mwenye asili ya Senegal, Akon. Akizungumza na Bongo5, Mayunga amesema kuwa bado hajaitwa na msanii yeyote kutoka Tanzania ili wafanye collabo.
“Bado sijafanya collabo yeyote na msasnii kutoka bongo na hakuna msanii yeyote mkubwa aliyenitafuta. Nafikiria watakuwa wanaogopa tu, mimi nipo tayari muda wowote kufanya nao,” aliongeza.
Aidha Mayunga amewatoa hofu mashabiki wake kwa kuwaambia kuwa bado kuna uwezekano mkubwa kwa yeye kufanya nyimbo nyingine mbili au hata zaidi na Akon.