» » Barabara ya Nyololo kujengwa kwa lami- Ngonyani

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini Mendrad Kigola (CCM) ameuliza swali Bungeni kuhusiana na barabara ya Nyololo, Kibao na Igolole kwamba ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami baada ya upembuzi yakinifu kukamilika mwaka 2013&2014.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Endwin Ngonyani amesema kwamba ukweli upembuzi yakinifu wa barabara hiyo umekamilika na serikali kwa sasa inatafuta fedha ili kuweza kujenga barabara hiyo kuanzia wakati wowote.

Naibu waziri huyo amekiri barabara hiyo kuwa kwenye ilani ya chama cha mapinduzi ukurasa wa 61 hivyo barabara hiyo itajengwa ili kuongeza kasi ya maendeleo katika ukanda huo.

-Aidha Mhandisi Ngonyani amesema kwamba TANROADS itaendelea kukarabati barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe hadi hapo fedha zitakapo patikana.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post