» »Unlabelled » Sheria ya habari kukwamisha ukusanyaji kodi

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Baadhi ya vifungu katika sheria mpya ya Huduma za Vyombo vya Habari vimebainika kuwa vinaweza kuchochea baadhi ya makampuni kushiriki katika mbinu chafu za kibiashara ikiwemo ukwepaji wa kodi.

Hali hiyo inatokana na vifungu hivyo kudhoofisha uandishi wa habari za kiuchunguzi, hasa zile zinazolenga kufichua uovu unaofanywa na makampuni hayo.

Hayo yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Wakili Mwandishi Bw. James Marenga, wakati wa mjadala wa wanahabari kuhusu sheria mpya ya huduma za vyombo vya habari, mjadala ulioandaliwa na ya taasisi ya habari ya Kimataifa ya Internews, kwa lengo la kuwapa waandishi nchini uelewa mpana wa maudhui ya sheria hiyo.

Serikali katika mjadala huo iliwakilishwa na Kaimu Msajili wa Magazeti Bw. Patrick Kipangula ambaye amesifu baadhi ya vifungu katika sheria hiyo kwa maelezo kuwa vitaboresha tasnia ya habari pamoja na maslahi ya waandishi wa habari nchini.

Awali katika maelezo yake, Mwezeshaji kutoka Internews na Mwandishi Mkongwe Bi. Alakok Mayombo amesema mjadala huo umelenga kuwawezesha wanahabari kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria hiyo pasipo kusuguana na serikali sanjari na kutoa mwanya wa kufanyia mabadiliko baadhi ya maeneo yanayoonekana kikwazo kwa kazi ya uandishi wa habari.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post