» »Unlabelled » Aliyetobolewa macho uso kwa uso na Scorpion mahakamani

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Wednesday, December 14, 2016

Tokeo la picha la scorpion mtoboa macho

Kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi inayomkabili Salum Njwete ‘Scorpion’ imeendelea katika mahakama ya wilaya ya Ilala wakati shauri hilo lilipoletwa kwa ajili ya kusikilizwa.

Picha inayohusiana

Wakati mshitakiwa akipandishwa kizimbani alidai ana wakili wake hivyo mahakama ilisubiri kwa muda wakili wa mshitakiwa Juma Nassoro na baada ya kufika mahakamani ndio kesi ilianza kusikilizwa.

Kesi hiyo ina mashahidi sita na mpaka sasa ameshasikilizwa mmoja ambaye ni shahidi namba moja Said Mrisho ‘aliyetobolewa macho’ ambaye leo December 14 2016 ametoa ushahidi wake mahakamani hapo akielezea tukio alilofanyiwa.

Baada ya kusikiliza kesi, mahakama hiyo imeahirisha shauri hilo hadi December 28 mwaka huu ambapo itaendelea na shahidi wa pili. 
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post