» »Unlabelled » NI KOSA LA JINAI KUTOMSAJILI MWAJIRIWA KATIKA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Ni  haki  ya  kila  mwajiriwa kuwa  amesajiliwa  na  mfuko  wa  hifadhi  ya  jamii.  Ni  jukumu  la  kila  muajiri  kuhakikisha  kila  mwajiriwa  wake  amesajiliwa  katika  mfuko  wa  hifadhi  ya  jamii.  Suala  la  mfanyakazi  kusajiliwa  katika  mfuko  wa  hifadhi  si  hiari  au  hisani  kwa  mwajiri.  Ni  lazima   afanye  hivyo kwa kuwa  ni  takwa  la  kisheria.  Wapo  wafanyakazi  wengi  wameajiriwa  kwa  mikataba  lakini  hawajasajiliwa  na mifuko  hii.  Kufanya  hivyo  ni  kukiuka  haki  ya  mfanyakazi.  Kusajiliwa  na  mfuko  wa  hifadhi  ni  katika  mambo ambayo  yanatakiwa  kufanywa  awali  kabisa  ajira  ya  mtu  inapoanza.
Ni  wajibu  wako  mfanyakazi  pia  kuhakikisha       unamkumbusha  mwajiri  wako  kufanya  hivyo  na/au  ikishindikana  waweza  kumchukulia  hatua.
JE? NI KOSA  LA  JINAI  KUTOMSAJILI  MWAJIRIWA  KATIKA  MFUKO  WA  HIFADHI.
Kwa mujibu wa Mwanasheria na msahauri wa Gazeti la serikali la Habari Leo Bashir Yakub amefanunua jambo hilo kuwa ukisikia  makosa  ya  jinai  ni  yale  makosa  ambayo  mtu  hushitakiwa  na  Jamhuri.  Ni makosa ambayo  mnatendeana wawili  lakini  anayeshitaki  ni  Jamhuri/Serikali. Ni makosa  ambayo  ukipatikana  na  hatia  adhabu  zake  huwa  ni  vifungo, faini  na  wakati  mwingine  kuchapwa  bakora.  Kwa  maana  hii  mwajiri  yeyote ambaye   amekataa  kumsajili  mfanyakazi  wake  katika  mfuko  wa  hifadhi  ya  jamii  anakuwa  ametenda  kosa  la  jinai  ambapo  anastahili  kuadhibiwa.
Kosa  hili  limeingizwa  katika  makosa  ya  jinai  kutokana  na  umuhimu  wa mifuko hii.  Lakini  pia ni  kutokana  na  ukweli  kuwa  waajiri  wengi  wasingependa  kuwasajili  waajiriwa  wao  kwa kuwa  wao  hutakiwa  kuchangia  asilimia  kadhaa  ya  fedha  kila  mwezi. Kwa kuwa  wasingependa  wachangie  fedha  hizi  ndio  maana  ikaingizwa  kwenye  jinai  ili  wa  kuogopa  na  aogope.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post