» »Unlabelled » Moto wawaka kashfa kontena 100 Bandari

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


MKURUGENZI WA TPA, DEUSDEDIT KAKOKO.

SIKU moja baada ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, kusema kontena 100 zimeondolewa Bandari ya Dar es Salaam bila kukaguliwa na Shirika la Viwango (TBS), moto kuhusiana na suala hilo umezidi kuwaka.

Hali hiyo imejidhihirisha kutokana na taarifa kuwa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) haikuhusishwa vya kutosha katika utoaji wa taarifa sahihi juu ya suala hilo huku TBS wakidai kuwa hadi kufikia jana, tayari wafanyabiashara 10 walishajitokeza kwao kwa nia ya kutoa maelezo.

Akiwasiliana na Nipashe jana, Mkurugenzi Mkuu wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko, alielezea kushangazwa na taarifa zilizoelezwa kuhusiana na kontena hizo.

Aidha, Kakoko alisema hali hiyo ya kutolewa maelezo bila kutaka taarifa kwao ni sawa na ‘kukwepa kupata taarifa sahihi kutoka sehemu sahihi’.

Source: nipashe
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post