» »Unlabelled » Baada ya Dogo Janja kutangaza kuoa, Madee afunguka haya

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO



Dogo Janja ambaye sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Kidebe’ amefunguka na kutangaza rasmi kuwa ana mpango wa kutaka kuoa na kusema kwamba muda si mrefu anaweza kuvuta jiko na kuweka ndani.

Dogo Janja alisema haya kupitia kipindi cha Planet Bongo ambacho kilikuwa kinarushwa moja kwa moja kutokea Manzese na kusema kuwa suala hilo lipo kwenye mchakato ila ni kweli ana mpango wa kuoa muda si mrefu.

‘Yah ni kweli nataka kuoa muda si mrefu nitavuta jiko hivyo siwezi kusema ni lini ila suala hilo lipo kwenye mchakato” alisema Dogo Janja.
Tokeo la picha la madee

Kwa upande wa Madee ambaye ni mlezi wa Dogo Janja kimuziki na katika maisha ya kila siku alisema kuwa kitendo cha Dogo Janja kutaka kuoa kabla yake itakuwa kama dharau hivyo anapaswa kusikilizia kwanza mpaka yeye afanye mambo kwanza ndipo na yeye atangaze.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post