Winnie Madikizela Mandela
Winnie ambaye alikuwa mkewe rais wa zamani wa taifa hilo Nelson Mandela na ambaye alipigana vita dhidi ya ubaguzi wa rangi, ameambia waandishi habari: ''Hatuwezi kujifanya kwamba hakuna matatizo''.
Amesema kuwa kuna vitu vingi ambavyo vimefanywa kimakosa na kwamba chama hicho kinahitaji uongozi mpya ili kushirikiana na viongozi wazee wa chama.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma
Matamshi yake yanajiri wakati ambapo mirengo tofauti ya chama hicho inakabiliana kuhusu kuimarisha uungwaji mkono wa chama hicho baada ya matokeo mabaya ya uchaguzi wa serikali za mitaa.