» »Unlabelled » Mgodi Mwadui wasababisha vilio

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Shinyanga. Kuanguka kwa mtambo baada ya Kamba iliyokuwa imeushikilia kukatika katiak Mgodi wa Williamson Petra Diamond Ltd mkoani Shinyanga, kumesbabisha vilio na simanzi kwa wafanyakazi na familia zao.

Wafanyakazi waliokufa kwa kuangukiwa na mtambo huo ni Benjamin Zephania (29) na Alex Mashenene (32) wote wakazi wa Mwadui, wilayani Kishapu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Muliro Jumanne alisema wafanyakazi waliokufa kwenye tukio lilitokea wakati wakirekebisha mashine.

Muliro alisema wafanyakazi hao walikuwa mafundi wa mgodi na kwamba, mtambo ulianguka baada ya kamba iliyokuwa imeushikilia kukatika.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post