» » Ufaransa yatinga fainali, Ujerumani nje

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO
Wachezaji wa Ufaransa wakishangilia ushindi

Ufaransa imetinga katika hatua fainali ya Kombe la Mataifa barani Ulaya kwa mwaka huu baada ya kuifunga Ujerumani 2 - 0.

Mshambuliaji Antoine Griezmann ndiye aliyeipeleka timu yake ya Ufaransa katika hatua fainali ya Kombe la Mataifa barani Ulaya kwa mwaka huu baada ya kuifungia magoli 2 na kuishangaza Ujerumani iliyokuwa imetawala mchezo huo wa nusu fainali.

Mshambuliaji huyo wa Atletico Madrid alianza kwa kuandika bao la kwanza kwa njia ya penalti katika dakika ya 45 kipindi cha kwanza kabla ya kupachika bao la pili na ushindi kipindi cha pili baada ya golikipa wa Ujerumani Manuel Neuer kufanya makosa golini.

Kwa matokeo hayo sasa Ufaransa mwenyeji wa michuano hiyo itakutana na Ureno katika mechi ya fainali siku ya Jumapili.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post