» » Serikali yatakiwa kutunga sheria kuzuia ngono kwa watoto

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Kahama.  Mkurugenzi wa asasi isiyo ya kiserikali ya Zovada, Endre Kibela ameishauri Serikali kutunga sheria ya kuwadhibiti watoto wote chini ya miaka 15 kutoshiriki ngono ili kujilinda na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU).

Akizungumza jana katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama amesema kama sheria hiyo itatungwa itawafanya watoto hao kutojihusisha na ngono kwa kuhofia kufungwa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti ukimwi katika halmashauri hiyo, Benedictor Manuari ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali kuhakikisha yanakuwa na takwimu sahihi za wagonjwa wa Ukimwi pamoja na kupeleka elimu ya kujikinga na maambukizi vijijini.

Amesema kama elimu hiyo itaendelea kutolewa kwa kasi, uwezekano wa kumaliza tatizo hilo ni mkubwa.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post