» » Watu 80 wauawa na radi nchini India

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


India radi

Maafisa nchini India wanasema kuwa watu 80 wameuwawa baada ya kupigwa na radi katika maeneo ya kaskazini na mashariki mwa taifa hilo katika muda wa saa 24 iliyopita.

Watu 53 walifariki katika jimbo la Bihar.Watu 10 waliuawa katika jimbo la mashariki la Jharkhand huku wengine 16 wakifariki katika eneo la Madhya Pradesh.

Wengi waliuawa walipokuwa wakifanya kazi katika mashamba yao wakati huu wa msimu wa mvua
Ni idadi kubwa sana ya watu kuuawa kwa mpigo mmoja ,jambo ambalo limewashangaza wengi.

Katika muongo uliopita, zaidi ya watu elfu mbili wamefariki kwa kupigwa na radi kote nchini India.

Ni vigumu sana kubashiri ni lini janga la radi litatokea na si rahisi kwa utawala kutoa tahadhari ya kutokea kwa radi.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post