
Mtu mmoja asiyefahamika aliyekuwa akiendesha baiskeli amefariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya kugongwa na gari aina ya Haice huku abiria zaidi ya kumi waliokuwa kwenye gari hiyo iliyokuwa ikitoka Songea kwenda Peramiho wakinunusurika kufa baada ya ajali hiyo iliyotokea maeneo ya Mfaranyaki mjini Songea mkoani Ruvuma.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema chanzo cha ajali hilo ni mwendo kasi uliomshinda dereva wa gari hilo ambapo alimgonga mwendesha baiskeli na kusababisha kifo chake na kisha kumjeruhi mwendesha boda boda aliyelazwa katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma.
Kufuatia ajali nyingi kutokea eneo hilo la Mfaranyaki katika daraja la Mkomi wananchi wameiomba serikali kuweka matuta kwenye eneo hilo ili kudhbiti mwendo wa madereva huku wakiwalalamikia madereva wanaokimbiza magari kwa ajili ya kuwahi abiria na kusababisha ajali.
ITV ilienda katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma kuwaona majeruhi wa ajali hiyo ambapo akizungumza kwa simu na ITV Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dk Philisy Nyimbi amesema waandishi hawaruhusiwi kuwaona majeruhi bila yeye kuwepo na kwamba muda huo haukuwa wa kazi huku Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Bw.Zuberi Mwombeji alipopigiwa simu yake ya mkononi alikuwa hapatikani....
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema chanzo cha ajali hilo ni mwendo kasi uliomshinda dereva wa gari hilo ambapo alimgonga mwendesha baiskeli na kusababisha kifo chake na kisha kumjeruhi mwendesha boda boda aliyelazwa katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma.
Kufuatia ajali nyingi kutokea eneo hilo la Mfaranyaki katika daraja la Mkomi wananchi wameiomba serikali kuweka matuta kwenye eneo hilo ili kudhbiti mwendo wa madereva huku wakiwalalamikia madereva wanaokimbiza magari kwa ajili ya kuwahi abiria na kusababisha ajali.
ITV ilienda katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma kuwaona majeruhi wa ajali hiyo ambapo akizungumza kwa simu na ITV Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dk Philisy Nyimbi amesema waandishi hawaruhusiwi kuwaona majeruhi bila yeye kuwepo na kwamba muda huo haukuwa wa kazi huku Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Bw.Zuberi Mwombeji alipopigiwa simu yake ya mkononi alikuwa hapatikani....
