» » Mbunge CCM alia kuvuliwa kofia

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Dodoma.Mbunge wa Ulanga (CCM), Gudluck Mlinga leo amemshtaki mbunge wa viti maalumu kutoka Chadema akidai kuwa amemdharirisha kwa mambo sita.

Mlinga alitoa kauli hiyo wakati akiomba mwongozo wa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson mara baada ya kipindi cha maswali na majibu, akisema mbunge wa Chadema, Anathopia Theonest alimvua kofia ya balaghashia aliyokuwa ameivaa.

Mlinga alidai kuwa mbunge huyo alifanya kitendo hicho wakati wabunge wa Ukawa walipokuwa wanatoka nje kuendelea na msimamo wao wa kususia vikao vinavyoendeshwa na Dk Tulia. Alidai kuwa Theonest alimfuata na kumvua kofia yake, ambayo kwa mujibu wa kanuni za Bunge ni lazima ivaliwe na kanzu.

Alisema kitendo hicho ni cha udhalilishaji, kimetikisa akili yake, kimevunja amri ya tisa ya kutamani mume wa mtu mwingine, kimewakosesha wananchi wa jimbo lao uwakilishi wa muda aliokuwa nje ya ukumbi na kimedhalilisha vazi hilo.



ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post