» » Maghembe aomba sapoti kukabili ujangili

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Dar es Salaam. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe ameomba Jumuiya  ya Kimataifa kuunga mkono juhudi za Serikali katika kupiga vita ujangili.

Profesa Maghembe amesema hayo leo, eneo la Matambwe Selous kwenye hafla fupi ya makabidhiano ya ndege maalumu nane zisizo na rubani zilizotolewa na Mfuko wa Uhifadhi Wanyamapori na Mazingira Duniani (WWF).

Ndege hizo zitatumika katika Pori la Akiba la Selous kuimarisha ulinzi wa wanyamapori kwa kukusanya taarifa za kiintelijensia, zitakazosaidia kukamatwa majangili. Ndege hizo zina thamani ya dola 80,000 za Marekani (Sh172 milioni).

“Msaada huu umekuja wakati mwafaka, Pori la Akiba la Selous linahitaji teknolojia za kisasa kuimarisha mapambano dhidi ya ujangili ndani na kuzunguka hifadhi hii,” amesema Proesa Maghembe.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post