» » Jamali Kisongo amevujisha picha za usajili-Poppe

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Moja ya picha iliyovuja mitandaoni ikionyesha kiungo wa Mtibwa Sugar Mohammed Ibrahim "MO" akisaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Simba kwa msimu ujao, na kushoto ni Rais wa Simba Evans Aveva akishuhudia kwa umakini

Mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu ya Simba Zakaria Hans Poppe, ameshusha lawama kwa Wakala wa wachezaji, Jamal Kisongo, kwa kuvujisha picha za usajili wa mchezaji anayemmiliki ambaye amesaini klabu hiyo, hivi karibuni.

Poppe, amesema kamati yake ilikubaliana zoezi hilo lifanyike kimya kimya na likikamilika ndiyo litangazwe, ili kuondoa wavurugaji wanao iharibia klabu hiyo.

Picha iliyovuja kwenye vyombo vya habari ni ya kiungo wa Mtibwa Sugar, Mohamed Ibrahim 'Mo', aliyeonekana akisaini karatasi za wekundu wa Msimbazi mbele ya Rais wa klabu hiyo Evans Aveva mwishoni mwa wiki iliyopita, ambapo awali Kisongo aliiomba picha hizo kwa kumbukumbu zake laini imekuwa sivyo.

Aidha kwa upande mwingine Poppe amesema hadi kufikia mwishoni mwa wiki hii, zoezi la wachezaji wa ndani litakuwa limekamilika na litakalofuata ni la wachezaji wa kimataifa ambao wanafanya nao mazungumzo hivi sasa.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post