» » HIMID MAO: GAME NGUMU, GAME MUHIMU, TUNATAKIWA KUPATA USHINDI

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO



Kiungo wa Stars na Azam FC Himid Mao ‘Ninja’ amesema, kila mchezaji wa Stars yupo tayari kwa ajili ta game ya kesho dhidi ya Misri.

shaffihdauda.co.tz imepiga story na kiungo huyo mkabaji mara baada ya mazoezi ya mwisho leso asubuhi ambaye amesema mchezo wa kesho utakua mgumu lakini ni mchezo muhimu kwa Stars kushinda.

“Game ni ngumu lakini ni game muhimu, mwisho wa siku inabidi tu-fight, tupambane na tupate matokeo”, amesema Himid ambaye kwa sasa anafanya vizuri kwenye nafasi ya kiungo wa ulinzi ambayo zamani ilitawaliwa na wachezaji wakongwe kama Shabani Nditi na Athumani Idd ‘Chuji’.

“Watu wote wako focused wana concentrate wako tayari kwa game, kwahiyo mchezaji atakayepata nafasi ataweza kufanya vizuri”.

Himid anaamini Stars itafanya vizuri kwenye mchezo wa kesho licha ya mchezo huo kuwa mgumu kutokana na nafasi ya Stars na Misri kwenye kundi.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post