» » #EURO2016: FULL RATIBA YA 16 BORA

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Baada ya mechi za makundi kumalizika jana, sasa inafuata hatua ya 16 bora ya michuano ya Euro 2016. Ni baada ya mechi kali na za kusisimua zilizoshuhudia Ureno na Ireland zikipenya dakika za mwisho .

Kuna mechi kadhaa ambazo zinaturudisha kwenye historia ya mashindano haya na zinatarajia kuwa na presha kubwa kuanzia kwa wachezaji, mabenchi ya ufundi na hata mashabiki pia.

Italy v Spain inatarajiwa kuwa mechi kali mchezo ambao unazirejesha timu hizo kwenye kumbukumbu ya mchezo wa fainali ya Euro 2012 ambao Spain walishinda kwa bao 4-0.

Spain pia iliifunga Italy kwenye michuano ya Euro 2008, kwa hiyo Italy vichwani mwao watakuwa na kibarua cha kulipa kisasi watakapokutana siku ya Jumatatu.

Ufaransa v Ireland ni game nyingine ianayotazamwa kwa uzito wa aina yake licha ya Ireland kuonekana kama vibonde mbele ya Ufaransa. Goli la mkono la Thierry Henry bado linawakumbusha machungu Ireland pale waliposhindwa kufuzu kucheza michuano ya kombe la dunia.

Ratiba kamili ipo kama ifuatavyo:

Switzerland v Poland (Jumamosi)

Wales v Northern Ireland (Jumamosi)

Croatia v Portugal (Jumamosi)

France v Republic of Ireland (Jumapili)

Germany v Slovakia (Jumapili)

Hungary v Belgium (Jumapili)

Italy v Spain (Jumatatu)

England v Iceland (Jumatatu)
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post