» » VIDEO..!!! Ben Pol: Nafurahi kuona wasanii wananiomba namba ya Lollypop aliyeuandika ‘Moyo Mashine

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO
Ben Pol amesema anafurahi kuona kuwa wasanii wengi wanamuomba namba ya mwandishi wa hit single yake ‘Moyo Mashine’ ili wafanye naye kazi pia.
13129947_1620670814901499_611261908_n
Wimbo huo umeandikwa na Lollypop ambaye pia aliandika nyimbo za Barakah Da Prince, Siachani Nawe na Nivumilie pamoja na Basi Nenda ya Mo Music.
“Sasa hivi kwanza nimepigisiwa simu na wasanii wengine wanaomba namba ya Lollypop,” Ben ameiambia Bongo5. “Hiyo ni kitu ambacho nilikuwa nataka kiwe hivyo,” ameongeza.
Ben Pol amesema tofauti na wasanii wengi, haoni kama ni kitu cha aibu kuandikiwa wimbo na mtu mwingine ambaye msanii atamtaja mara zote. Amedai amegundua kuwa sifa zote za uzuri wa wimbo huo anazipata yeye kama muimbaji hivyo hakuna kitu cha kuonea aibu kuandikiwa nyimbo.


“Hamna weakness ambayo naificha au labda nikautoa ule wimbo nikaficha baadhi ya details. Watu wengi wanafanya hivyo, wengi sana na nyimbo kubwa kweli, mtu anatoa nyimbo lakini hazungumzii kipengele cha nani kaandika, anazungumzia mambo mengine tu.”
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post