» » Global FC, Kili Vetereni kutoana roho leo

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


KIKOSI cha timu ya Global FC, leo Ijumaa kinatarajia kushuka dimbani kumenyana na timu ya Kili Veterani katika mchezo spesho wa kirafiki ambao unatarajiwa kupigwa katika Uwanja wa Kili, Kunduchi jijini Dar.

Mchezo huo ambao unatarajiwa kuwa na upinzani wa hali ya juu, pia utatumika katika kuitangaza promosheni ya Bahati Nasibu ya Jishindie Nyumba ambayo inaendeshwa na gazeti hili sambamba na magazeti mengine ya Global Publishers.

Nahodha wa Global FC, Philipo Nkini, ameliambia Championi Ijumaa kuwa licha ya mchezo huo kuwa wa kirafiki, lakini wao wanauchukulia kwa uzito.

“Huu ni mwanzo wa michezo yetu ya kirafiki ambayo kwa kipindi hiki itakuwa kila mara ambapo tumejiandaa vziuri kukabiliana na wapinzani wetu ambapo pia mchezo huu tutakuwa na kitengo chetu cha usambazaji ambacho kitadili na kuitangaza bahati ya Shinda Nyumba,” alisema Nkini.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post