» » Avimba Tumbo Miaka 21

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Amina Ahmad.
Na Imelda Mtema, UWAZI
Mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la  Amina Ahmad (45) mkazi wa Magomeni Chama jijini Dar, yuko katika mateso makali sana kwa muda wa miaka 21 baada ya uvimbe uliokuwepo tumboni kumsumbua huku akiwa hajaweza kwenda hospitali hata siku moja.
Akizungumza na gazeti hili kwa uchungu mama huyo amesema tatizo hilo lilimuanza tangu 1995, ambapo kilianza kitu kama kipele kidogo lakini siku zilivyozidi kusonga kikawa kinaongezeka lakini alikuwa akiona ni hali ya kawaida.
“Mara ya kwanza niliona ni jambo la kawaida sana lakini siku zilivyosonga ndivyo nilivyoona kinazidi kukua kitu ambacho kilianza kunipa shaka kidogo,” alisema Amina.
gonjwa la tumbo (1)
Mgonjwa huyo aliendelea kuzungumza kuwa maisha yake ni duni sana  hana kipato chochote cha kumuwezesha kwenda kutibiwa hospitali kwa kuwa anajua ataambiwa inapaswa kufanyiwa upasuaji wakati hana uwezo wa fedha kwani hela anayopata kwa siku ni ndogo sana tena ya mlo mmoja.
“Yaani natamani sana hospitali hata wajue hili tatizo lakini sina hela hata ya kuanzia kwa sababu kipato changu ni cha chini sana tena cha mlo mmoja tu na wakati mwingine usiwepo,” alisema.
Aliendelea kusema kuwa amekuwa mtu wa kulala kwa kuwa hawezi kufanya kazi nzito kwa sababu ya maumivu makali anayopata na kuna wakati anatapika mpaka kupoteza nguvu na kuanguka chini ambapo husaidiwa na mwanaye wa miaka tisa.
“Kwa jinsi uvimbe huu unavyonitesa nahisi siku moja utapasuka na kusababisha nikapoteza maisha na kumuacha mwanangu akiteseka kama mimi mama yake,” alisema Amina kwa huzuni.
Msomaji wetu, Amina yupo katika mateso makali hivyo anaomba msaada wako ili aweze kwenda hospitali kupata matibabu kisha aendelee na shuguli zake za kila siku akiwa mwenye afya njema na furaha kama wewe.
Kama umeguswa na tatizo lake unaweza kumtumia mchango wako kupitia namba zake ambazo ni 0716 416144 au 0783414944 na Mungu atakubariki.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post