» »Unlabelled » Operesheni ya kupima ulevi kwa madereva yahamia Mwanza.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Mwanza kwa ushirikiano na maofisa wa mamlaka ya udhibiti usafiri wa nchi kavu na majini( SUMATRA ) mkoani humo,wamefanya ukaguzi wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri wa abiria mikoani na nchi jirani,ikiwemo kupima kiwango cha ulevi kwa madereva wa mabasi hayo na kuwataka abiria kupaza sauti pale wanapoona dereva anaendesha gari kwa mwendo wa kasi.

Ukaguzi huo umefanyika hii leo alfajiri katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani ya Uganda kilichopo Nyegezi jijini Mwanza, ambapo Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoani hapa Mrakibu Mwandamizi wa polisi Robert Hussein aliongoza zoezi hilo la kupima kilevi kwa madereva wa mabasi,ukaguzi wa mabasi ya abiria na kutoa elimu kwa abiria kuhusu wajibu na haki zao wanapokuwa safarini.

Peter Rusibamayila ni balozi wa usalama barabarani mkoani Mwanza anasema kazi kubwa waliyonayo ni kuwaelimisha abiria ili waweze kupaza sauti, kutambua haki na wajibu wao ikiwemo kufunga mkanda kwa lengo la kupunguza ajali zinazoweza kuepukika,huku baadhi ya abiria na madereva wakishauri kuwa zoezi hilo linapaswa kuwa endelevu.


ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post