» » Mtanzania adaiwa kumdhalilisha mtumishi wa ndege

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 42 anashikiliwa na Mahakama Kuu ya makosa ya jinai ya jiji la Dubai, Falme za Kiarabu kwa tuhuma za kumdhalilisha mhudumu wa kike wa Shirika la Ndege la Emirates.

Raia huyo ambaye jina lake limeandikwa kwa herufi za mwanzo za MA, anasubiri kesi yake kusikilizwa Julai 24, mwaka huu.

Mtanzania huyo anadaiwa kumdhalilisha mhudumu huyo mwenye umri wa miaka 25  wakati wakiwa wanasafiri na ndege hiyo kutoka Dar es Salaam kwenda Dubai, Aprili 24 mwaka huu.

Kwa mujibu wa habari iliyochapishwa juzi kwenye mtandao wa shirika hilo la ndege unaoitwa, Emirates 24/7, Mtanzania huyo alimwomba mhudumu huyo wapige picha ya pamoja kwa ajili ya ukumbusho.

Mhudumu huyo ambaye pia jina lake halikutajwa, alikubali.

“Wakati anapiga picha aliniwekea mkono kwenye bega. Kiongozi wangu aliona na kumuonya. Baada ya kuona hivyo, akaomba tupige selfie,” amesema mhudumu huyo.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post